Dhuluma kama kichocheo cha mzinduko wa wanawake katika riwaya ya kiswahili

Loading...
Thumbnail Image

Date

2018-11

Authors

Mboya, Lucy A.
Mohochi, Sangai
Kisurulia, Simiyu

Journal Title

Journal ISSN

Volume Title

Publisher

International Journal of Social Sciences and Information Technology

Abstract

Kwa kipindi kirefu wanawake wametwezwa na kudunishwa kutokana na dhuluma wanazofanyiwa na jamii inayotawaliwa na mfumo wa kuumeni. Dhuluma wanazopata wanawake zinatokana na asasi tofauti tofauti ambazo ndizo zinapaswa kudumisha mshikamano wa kijamii. Tahakiki na tafiti nyingi zinaonyesha athari ya ukandamizaji wa jinsia ya kike na hali ya kuzimwa kwa juhudi zake katika kupigania nafasi yake. Mwanamke anavyoitikia hali hii kwa njia inayomzindua na kumfaidi ni suala ambalo halijaangaziwa pakubwa. Ni kutokana na msingi huu ambapo makala hii inachunguza namna dhuluma wanazopata wanawake zinavyowazindua na kuwapa motisha ya kujikomboa na kujinasua kutokana na hali hii ya kusakamwa na asasi kandamizi za kijamii. Kwa njia hii, wanawake wanapata nafasi ya kujiendeleza katika nyanja mbalimbali ikiwemo kujieleza kimapenzi badala ya kuridhia kuishi vivulini mwa waume zao dhalimu. Hali hii inampa mwanamke taswira mpya kama kiumbe mwenye thamani na mchango mkubwa katika kuongoza juhudi za ufanisi wa jamii yake. Uchunguzi huu umeegemea fasihi andishi ya Kiafrika kwa kurejelea kazi mbili: Nyuso za Mwanamke (Mohamed, 2010) na Heri Subira (Babu, 2010). Riwaya hizi ziliteuliwa kwa kutumia mbinu ya uteuzi wa kimakusudi. Riwaya hizi zimesheheni hali ngumu ya maisha wanayopitia wahusika wa kike hasa katika harakati zao za kujinasua kiuchumi na kujisaka kimapenzi. Aidha zimeangazia masuala ya wanawake kwa uangavu na kwa namna inayopanua nafasi ya jinsia ya kike katika dunia ya kisasa. Kutokana na mchango mkubwa wa wanawake katika shughuli mbalimbali za ujenzi wa jamii, ni bayana kuwa matumizi ya fasihi

Description

Keywords

kama wenzo wa kuwazindua wanawake kijamii ni hatua muhimu katika maendeleo ya jamii.

Citation